• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • muudo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Idara
        • Afya
          • Wasifu wa Idara ya Afya
          • Taarifa ya utekelezaji Afya
        • Elimu Msingi
        • Utumishi na utawala
        • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
        • Maji
        • Ardhi na Maliasili
        • Ujenzi
          • Wasifu wa Idara
          • Taarifa ya utekelezaji
        • Fedha
        • Elimu Sekondari
        • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Vitengo
        • Habari,Mawasiliano,TEHAMA na Uhusiano
        • Ukaguzi wa ndani
        • Nyuki
        • Biashara
          • Utaratibu wa utoaji wa leseni
        • Mifugo na uvuvi
        • ununuzi na ugavi
        • Sheria
          • Sheria ndogo za halmashauri
          • Sheria m alimbali
      • Machapisho ya Idara
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya watalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayo tekelezwa
    • Miradi inayoendelelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

Watendaji Nsimbo watakiwa Kujizatiti ukusanyaji mapato

Imewekwa: April 20th, 2017



Na:John A.Mganga( I.O Nsimbo DC )

Watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo wametakiwa kujidhatiti katika kudhibiti mapato ya Halmashauri ili kuondoa uwezekano wa kupoteza mapato katika maeneo mbalimbali ya ukusanyaji wa mapato katika Halmashauri hiyo.

Akizungumza wakati wa Ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Madiwani Aprili 20 2017 Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo na Diwani wa Kata ya Machimboni Mh.Raphael Kalinga amesema jitihada za makusudi zinahitajika kuhakikisha kuwa mapato ya Halmashauri yanadhibitiwa ipasavyo jambo litakalosaidia kuboresha mapato na kuondokana na tatizo la uhaba wa fedha unaochelewesha kukamilika kwa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Mwenyekiti amewataka watendaji wa Halmashauri  Nsimbo kuwa wabunifu katika kubuni vyanzo mbalimbali vya mapato vitakavyowezesha Halmashauri kuongeza mapato jambo litakalosaidia kwa kiasi kikubwa kufikia malengo ya Halmashauri ya kuwaletea wananchi Maendeleo.

Aidha Mwenyekiti huyo pia ametumia nafasi hiyo kuwataka watendaji wa Kata na Vijiiji kuwajibika ipasavyo kwa nafasi zao ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa Taarifa za Utekelezaji za Kata zinaandaliwa na kufikishwa katika Vikao vya Baraza la Madiwani mapema jambo litakalosaidia kujadili kwa wakati Taarifa hizo huku akisisitiza kutosita kuchukua hatua za kinidhamu kwa Madiwani ambao watashindwa kufikisha Taarifa za Utekelezaji wa Kata zao kikaoni.

Mwenyekiti huyo katika kutilia mkazo kile  anachozungumza na  anachokisimamia ametoa adhabu kwa kuwatoa nje  Diwani wa Kata ya Kapalala Mh.Reward Sichone pamoja na Diwani wa Kata ya Katumba Seneta Baraka Jetty, kutokana na kushindwa kuwasilisha kwa wakati Taarifa za Utekelezaji za Kata zao Kikaoni ambapo madiwani hao waliheshimu maamuzi ya Mwenyekiti wao na kukubali adhabu iliyotolewa.

Kalinga amekemea vikali tabia ya kutokuwasilisha Taarifa za Vikao kwa wakati na kuwataka  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri  ya Wilaya ya Nsimbo pamoja  na Afisa Utumishi kufuatilia kwa karibu kubaini chanzo cha tatizo hilo na kwamba hatua za kinidhamu zichukuliwe kwa wanaokwamisha Uandaaji wa Taarifa kwa Wakati.

Kalinga pia amewataka madiwani kushirikiana kwa karibu sambamba na  kuboresha mahusiano mema  na Wataalamu wa Halmashauri katika kata zao jambo litakaloboresha utendaji kazi wenye kuleta tija kwa Halmashauri kiujumla.

Mkutano wa Baraza la Madiwani halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo umefunguliwa leo kwa Madiwani kuwasilisha  Taarifa mbalimbali za Utekelezaji za  Kata ambapo kikao hicho kitamalizika Aprili 21 mwaka 2017.

Matangazo

  • NAFASI ZA MASOMO TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO April 08, 2018
  • TANGAZO LA AJIRA NSIMBO DC March 15, 2018
  • TANGAZO LA KIUTWA KAZINI March 23, 2018
  • SALAMU ZA PASAKA March 30, 2018
  • Angalia zote

Habari mpya

  • Madiwani Nsimbo wajengewa uelewa Kanuni za kudumu za Halmashauri.

    March 29, 2018
  • Maafisa Elimu Kata ,Walimu wakuu wa shule watakiwa kutimiza wajibu wao

    March 28, 2018
  • TEHAMA kuongeza kasi ya Utendaji kazi Nsimbo

    March 25, 2018
  • Wananchi Kanoge wapata neema ya Gari la Wagonjwa.

    March 24, 2018
  • Angalia zote

Video

Zoezi la Pigaji chapa Lilivyofanyika Nsimbo
Video zaidi

Quick Links

  • Orodha ya waheshimiwa madiwani
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Video mbalimbali
  • Muundo wa Halmashauri
  • Picha mbalimbali
  • Fomu mbalimbali

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : +255785659744

    Simu: +25585659744

    Barua pepe: info@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa