• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • muudo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Idara
        • Afya
          • Wasifu wa Idara ya Afya
          • Taarifa ya utekelezaji Afya
        • Elimu Msingi
        • Utumishi na utawala
        • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
        • Maji
        • Ardhi na Maliasili
        • Ujenzi
          • Wasifu wa Idara
          • Taarifa ya utekelezaji
        • Fedha
        • Elimu Sekondari
        • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Vitengo
        • Habari,Mawasiliano,TEHAMA na Uhusiano
        • Ukaguzi wa ndani
        • Nyuki
        • Biashara
          • Utaratibu wa utoaji wa leseni
        • Mifugo na uvuvi
        • ununuzi na ugavi
        • Sheria
          • Sheria ndogo za halmashauri
          • Sheria m alimbali
      • Machapisho ya Idara
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya watalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayo tekelezwa
    • Miradi inayoendelelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

Madiwani Nsimbo wajengewa uelewa Kanuni za kudumu za Halmashauri.

Imewekwa: March 29th, 2018


Pichani:Katibu  wa CCM Mkoa  wa Katavi Kajoro Vyohoroka akizungumza  wakati wa ufunguzi wa semina kwa madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo iliyofanyika leo Machi 29 kwa lengo la kuwajengea uelewa kuhusu Kanuni za Kudumu za Halmashauri(Picha na John Mganga)

 

 

Madiwani kutoka Kata 12 za Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo leo Machi 29 2018 wamepatiwa Semina ya siku moja ya kuwajengea uelewa wa Kanuni za Kudumu za Halmashauri

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Bw.Mwailwa Smith Pangani amesema Semina hiyo ya siku moja  imeandaliwa kwa lengo la kuwajengea uelewa Madiwani kuhusu  Kanuni za Kudumu  za Halmashauri ili kuwawezesha kutekeleza majukumu yao ya usimamizi wa shughuli mbalimbali katika kata zao kwa kuzingatia Kanuni Sheria na Taratibu za Halmashauri.

Akifungua Semina hiyo ya siku moja ,Katibu wa CCM Mkoa wa Katavi Kajoro Vyohoroka   amesema Mafunzo ya Kanuni za Kudumu za Halmashauri yatawasaidia madiwani kuwa na uelewa wa kutosha na hivyo  kushirikiana kwa karibu na Wataalamu wa Halmashauri yao katika kutekeleza shughuli mbalimbali za Kimaendeleo.

Amesema mafunzo hayo yamekuja kwa wakati muafaka kwani yatasaidia madiwani hao kuwa na uelewa  kuhusu taratibu za uendeshaji wa vikao  mbalimbali vya Halmashauri jambo litakalowasaidia Madiwani hao kufuata utaratibu.

Amesema ni jukumu la Madiwani kuhakikisha kuwa wanajenga mahusiano mema baina yao pamoja na kushirikiana kwa karibu na Wataalamu wa Halmashauri ambapo kufanya hivyo kutasaidia kwa sehemu kubwa kutekeleza kwa ufanisi shughuli mbalimbali za maendeleo na hivyo kufikia lengo la Serikali la kuboresha huduma za jamii kwa Wananchi

Bw.Kajoro pia amesisitiza kuwepo na utaratibu wa kutoa mrejesho kwa wananchi kwa kutumia njia mbalimbali za kuwafikia wananchi zikiwemo mbao za matangazo katika Ofisi za Kata ama katika mikutano yao ya hadhara jambo litakalosaidia wananchi kujenga imani na serikali

Ameongeza kuwa ni vema madiwani wa Halmashauri wakawa na kauli moja badala ya kutofautiana kimtazamo pindi wanapotoka nje jambo linalowachanganya wananchi na hivyo kuwafanya wananchi kutokuwa na Imani na Viongozi waliowachagua

Pamoja na mambo mengine amewataka madiwani na wataalamu kutambua kuwa mahusiano kati ya chama na Serikali ni muhimu kwa kuwa wataalamu wanatekeleza Ilani ya chama kilichopo madarkani hivyo ni muhimu kuboresha mahusiano mema na chama kilichopo madarakani kufikia lengo la utoaji huduma bora  kwa wananchi

Amesema ikiwa  madiwani watakuwa na mahusiano mema na wataalamu itasidia kwa sehemu kubwa madiwani kueleweshwa na kupewa ufafanuzi wa mambo mbalimbali yanayowatatiza jambo litakalowasaidia kuleta tija katika utendaij kazi.

Kwa upande wao madiwani waliopatiwa mafunzo hayo wameipongeza Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji kwa kuandaa semina hiyo ambapo wamesisitiza mafunz hayo kuwa endelevu ili kuwajengea uelewa zaidi.

Matangazo

  • NAFASI ZA MASOMO TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO April 08, 2018
  • TANGAZO LA AJIRA NSIMBO DC March 15, 2018
  • TANGAZO LA KIUTWA KAZINI March 23, 2018
  • SALAMU ZA PASAKA March 30, 2018
  • Angalia zote

Habari mpya

  • Madiwani Nsimbo wajengewa uelewa Kanuni za kudumu za Halmashauri.

    March 29, 2018
  • Maafisa Elimu Kata ,Walimu wakuu wa shule watakiwa kutimiza wajibu wao

    March 28, 2018
  • TEHAMA kuongeza kasi ya Utendaji kazi Nsimbo

    March 25, 2018
  • Wananchi Kanoge wapata neema ya Gari la Wagonjwa.

    March 24, 2018
  • Angalia zote

Video

Zoezi la Pigaji chapa Lilivyofanyika Nsimbo
Video zaidi

Quick Links

  • Orodha ya waheshimiwa madiwani
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Video mbalimbali
  • Muundo wa Halmashauri
  • Picha mbalimbali
  • Fomu mbalimbali

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : +255785659744

    Simu: +25585659744

    Barua pepe: info@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa