• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

Kilimo; KIBOWAVI kuchagiza kilimo cha Mbogamboga na Matunda Nsimbo.

Imewekwa: October 17th, 2020

Nsimbo -Katumba

Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo ni miongoni mwa Halmashauri 3 za Mkoa wa Katavi na Halmashauri 11 za Mikoa ya Nyanda za juu kusini  zinazotarajia kunufaika na  Mradi wa Kilimo bora cha Mboga mboga na matunda kwa Wanawake na Vijana KIBOWAVI.

Mratibu Mradi wa KOBIWAVI Mkoa wa Katavi Bw.Christopher Chaula ameeleza kuwa lengo kuu la Mradi huo wa Shirika la HELVETAS Tanzania  utakaotekelezwa kwa miaka minne kuanzia Februari 2020 hadi Februari 2024 kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya,  ni kuchangia katika ukuaji wa uchumi  jumuishi, kuendeleza sekta binafsi na kuzalisha ajira katika mnyororo wa thamani wa mazao ya mbogamboga na matunda pamoja na kuongeza usalama wa chakula na Lishe katika nyanda za juu kusini mwa Tanzania.

Akizungumza na Wananchi wa Kata ya Katumba eneo la Mnyaki Sokoni katika Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Chakula Duniani 16 Oktoba 2020 Chaula ameeleza kuwa utekelezaji wa Mradi huo kwa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo  unatarajia kuanza rasmi mapema 2021 ambapo utatekelezwa katika Kata 7 za Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo ambapo vikundi 100 vya Ujasiriamali vya Wanawake na Vijana vinatrajia kunufaika na Mradi huo.

Chaula amesema,Mradi wa KIBOWAVI kwa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo unatarajia kutekeleza shughuli zake za kuchagiza kilimo cha mbogamboga na matunda  katika Kata 7 ambapo utekelezaji wake utaanza kutekelezwa kupitia Vikundi vya Wanawake na Vijana vya Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo vinavyojihusisha na Kilimo cha Mboga mboga na matunda.

Ameeleza kuwa Mradi huo utaanzisha  mashamba darasa ya Kilimo cha Mbogamboga na matunda ili kutoa elimu kwa wakulima juu ya namna bora ya kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao ya Mbogamboga na matunda Nsimbo lengo kuu likiwa ni kuchangia katika ukuaji wa uchumi jumuishi na kuzalisha ajira katika mnyororo wa thamani wa mazao ya mbogamboga na matunda.

Aidha Chaula amesema Elimu juu ya mbinu bora za Kilimo cha mbogamboga na matunda itatolewa kwa wakulima Viongozi wa mazao ya mbogamboga na matunda Nsimbo ambapo kupitia Wakulima Viongozi hao wazalishaji watapata elimu ya namna ya kulima mazao ya matunda na mbogamboga.

Chaula pia ameeleza kuwa KIBOWAVI imedhamiria kujenga uwezo kwa wazalishaji wa matunda na mbogamboga ili waweze kuweka na kukopa kupitia vikundi vyao vya uzalishaji wa mazao ya matunda na mbogamboga.

Mradi wa Kilimo bora cha Mbogamboga na matunda kwa Wanawake na Vijana KIBOWAVI ni moja kati ya Miradi inayotekelezwa na Shirika la HELVETAS Tanzania Nchini  ukifadhiliwa na Umoja wa Ulaya kwa silimia 90 ambapo Asilimia 10 unafadhiliwa na Mshirika kiongozi HELVETAS Tanzania ambapo washirika wengine wa KIBOWAVI ni Shirika la CODERT,ADP Mbozi,na TAFOPA.

Matangazo

  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUANZA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021 KUTOKA NSIMBO-DC December 19, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOPENDEKEZWA KUJIUNGA MAFUNZO YA UFUNDI STADI CHUO CHA VETA MPANDA NA CHUO CHA MAENDELEO YA WANANCHI MSANGINYA MWAKA 2021 December 20, 2020
  • KATAZO LA MIFUKO YA PLASTIKI May 20, 2019
  • ACHANA NA MIFUKO YA PLASTIKI May 20, 2019
  • Angalia zote

Habari mpya

  • Wananchi Nsimbo punde kuhudumiwa katika Hospitali ya Wilaya.

    January 06, 2021
  • RC Katavi aipongeza Nsimbo kwa Usimamizi mzuri wa Miradi

    January 05, 2021
  • Madiwani Nsimbo wahimizwa kuhamasisha Wananchi kujiunga na CHF iliyoboreshwa.

    December 23, 2020
  • Naibu Waziri TAMISEMI aipongeza Nsimbo kwa harakati za Ujenzi wa Sekondari.

    December 15, 2020
  • Angalia zote

Video

Mwenyekiti Nsimbo akemea Uchangiaji holela wa vyombo vya kunywea pombe vilabuni
Video zaidi

Quick Links

  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa
  • Orodha ya waheshimiwa madiwani
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Video mbalimbali
  • Muundo wa Halmashauri
  • Picha mbalimbali
  • Fomu mbalimbali

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : +2552955164

    Simu: +255713992124

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa